Follow CHRIS MAUKI:

www.chrismauki.com

Thank you very much for visiting our blog. We have new website for you,we are sure this new website will completely blow your mind! Subscribe by entering your e-mail below to stay updated on our progress.

Launching
comeback
launchpad

Monday 12 May 2014

NI MTAZAMO TU KUHUSU PESA

Pesa, fedha au hela ni kati ya kitu cha ajabu sana ulimwenguni kinachoweza kusababisha furaha na wakati huo huo kusababisha huzuni, aliyenayo anajisikia furaha wakati asiye nayo anajisikia huzuni, pesa hii pia hubadilika badilika majina yake na sifa zake kutokana na mazingira au kazi inayofanya, kwamfano pesa hii ikiwa inalipwa serikalini inaitwa kodi “tax”, ila ikiwa inalipwa kwa mwenye nyumba inaitwa kodi ya nyumba “rent”. Pesa hii hii ikilipwa shuleni au chuoni inabadili jina inaitwa ada, wakati ikipelekwa kanisani kutolewa kama kawaida inaitwa sadaka na kama inatolewa kama sehemu ya kumi ya hela nyingine uliyoipata inaitwa fungu la kumi au “tenth”. Pesa hii pia akipelekewa baba mkwe kwa makusudio ya kumposa mtoto wake itaitwa mahari, wakati ikifika kwenye msiba inabadili jina na kuitwa rambi rambi. Mtoto akipewa na mzazi wake pesa itaitwa fedha ya mfukoni “pocket money” wakati mzazi wa mtoto huyu anapopewa pesa hii na mwajiri inatambulika kama mshahara. Mwanaume akimpa mpenzi wake noti hii hii ataonekana kuwa anajali, lakini akimpa mwanamke mwingine kwa nia ya kuhitaji mapenzi hataonekana kuwa anajali tena bali anahonga na mbaya zaidi huyu anayepokea pesa hii katika hatua hii haitwi tena ampenzi bali malaya. Ikiwekwa sehemu hela hii, mtu akichukua pasipo wengine kujua anaitwa mwizi, na kama aliyeichukua ni mtoto mdogo na ndio anaanza tabia ya kuchukua mara moja moja yeye wanamwita mdokozi, akizoea udokozi huu ndiyo watamwita mwizi, lakini endapo hela hii inachukuliwa kwa nguvu na mabavu, anayeishukua haitwi tena mdokozi wala mwizi bali anaitwa jambazi. Yani hii hela hii ni au ibadili jina lake kutokana na mazingira inavyotumika au ikubadili jina lako wewe kwa jinsi unavyoitumia. Na huu ni mtazamo tu – Chris Mauki

No comments:

Post a Comment

KWA USHAURI ZAIDI

Email : chrismauki57@gmail.com
Mob No:+255713 407182

Total Pageviews

TANGAZA NASI

TANGAZA NASI
+255718-243339 or +255713-407182 / chrissmauki2014@gmail.com
Powered by Blogger.

JITAMBUE KISAIKOLOJIA

JITAMBUE KISAIKOLOJIA

Popular Posts

About Me

Blog Archive