Follow CHRIS MAUKI:

www.chrismauki.com

Thank you very much for visiting our blog. We have new website for you,we are sure this new website will completely blow your mind! Subscribe by entering your e-mail below to stay updated on our progress.

Launching
comeback
launchpad

Thursday 8 May 2014

KWA WALE YENYE FAMILIA ZENU

Sikatai kabisa kwamba mara nyingi tunakuwa bize sana kama wazazi, tukijishuhulisha na yale yote ambayo yatazisaidia familia zetu kuiona kesho njema, yamkini baba yuko bize na mama hali kadhalika, muda wakuonana au hata kukaa kuongea na watoto wetu unakuwa kitendawili na bado tunaona “it is ok while it is not”. Nashauri hata kama mmejikuta mko bize kuliko mchwa, ni vema mkajitahidi kuwa na wakati wa kula pamoja kama familia. Nirahisi sana mkawepo pamoja kama familia lakini ukajikuta wewe baba labda hata wewe mama miezi imepita haujawahi kukaa mezani kula na wanao. Wengine watapelekewa chakula chumbani, wengine baba anakula pekeyake kwenye kochi, watoto wako kilomita mbili mbali, wengine watoto wanaanza kula kwanza na wazazi wanafuatia, hali zote hizi hazileti mwanya wa kujenga ukaribu baina ya wazazi na watoto. Ipo siri kubwa sana kwenye kukaa pamoja mkila kama familia, kuna vitu vingi sana unaweza kuvisoma kwa mwanao mkiwa mezani mnakula, viko vijitabia vilivyofichika vinaweza kusomeka mnapokuwa mezani na wanao, waweza pia kugundua hali ya mahusiano baina yao wenyewe unapokuwa pamoja nao mezani. Hivi vyote ni ngumu kudhihirika mkiwa meza za mahotelini na kwenye mitoko siku za sherehe, meza ya chakula ya nyumbani mwako ndio eneo muafaka. Hapa ndipo unaweza kufanya “check in” kwa watoto wako kama nilivyoizungumzia kwenye cd yangu ya “Jinsi ya kumlea na kumkuza mtoto mwenye furaha”. Wazazi wengi hatuwajui watoto wetu ingawa tumewazaa sisi wenyewe kwasababu tunakosa nyakati za maana na za muhimu kama hizi ninazozielezea hapa. Wazazi, jifunzeni kujenga panapostahili kujengwa, ili msije kubomoa pasipostahili kubomolewa – Chris Mauki

No comments:

Post a Comment

KWA USHAURI ZAIDI

Email : chrismauki57@gmail.com
Mob No:+255713 407182

Total Pageviews

TANGAZA NASI

TANGAZA NASI
+255718-243339 or +255713-407182 / chrissmauki2014@gmail.com
Powered by Blogger.

JITAMBUE KISAIKOLOJIA

JITAMBUE KISAIKOLOJIA

Popular Posts

About Me

Blog Archive